Sunday 17 April 2016

Hans awaonya waandishi wanaomchonganisha na Yanga

Kocha mkuu wa Yanga amelalamika juu ya waandishi ambao wamekuwa wakiandika vitu ambavyo yeye hajazungumza kwasababu vinamletea matatizo na waajiri wake.
Hans amesema hivyo baada ya gazeti moja kutoa habari ambayo inasababisha mazingira magumu, anasema yeye ni mwajiriwa hivyo anatarati zake  za kazi na badala yake amewaomba waandishi kuchukua na kufanyia kazi kile ambacho anakuwa amekizungumza mwenyewe
“Mimi huwa zizungumzi kuhusu kuhusu makocha, timu nyingine wala TFF, kuna gazeti linasema mimi nilienda TFF kujaribu kubadilisha tarehe za baadhi ya mechi lakini kulikuwa hakuna uwezekano juu ya hilo kwahiyo nikawa nimekasirishwa na TFF na kuanza kuwashutumu kwamba hawajui kufanya mambo yao, sijawahi kuzungumza kuhusu federation watu wanatakiwa kujua hilo”, amesema Hans ambaye anaonekana kuchukizwa na habari hiyo.

Kuhusu mchezo wao wa kiporo dhidi ya Mtibwa Sugar ambao Yanga walishinda kwa bao 1-0 na kukwea hadi kileleni mwa ligi, Hans amekimwagia sifa kikosi chake kuwa kimecheza vizuri kwenye mchezo huo licha ya kupoteza nafasi nyingi za kufunga magoli.
“Tulicheza vizuri sana kitu kimoja kilichotuangusha ni kutotumia nafasi tulizozipata, na wakati mechi inaelekea kumalizika kulikuwa na ‘tension’ kubwa kwa wachezaji wangu na hiyo ilisababishwa na kuwa na goli moja tu mkononi lakini kama unamagoli zaidi ya mawili unakuwa huna presha”.
“Tumecheza dhidi ya timu ngumu na tulilijua hilo kabla ndiyo maana mwanzoni tulianza na mfumo wa 3-5-2 lakini kwasababu tupo nyumbani na ni lazima tushinde mechi ndiyomaana tukamtoa beki mmoja nje na kuongeza mshambuliaji mwingine”.

No comments: