Tuesday 31 May 2016

Hivi ndivyo alivyookolewa Alan Pulido

Image result for alan pulidoMamlaka nchini Mexico wameelezea namna mchezaji wa kimataifa Alan Pulido alivyookolewa baada ya kutekwa nyara mwishoni mwa juma.
Maofisa wanasema kuwa muda mchache baada ya kutekwa kwake Pulido alipambana na mmoja wa watekaji wake na kumyang'anya simu yake kisha akawapigia polisi.
Pulido, anayechezea klabu ya soka ya Olympiakos ya Ugiriki alijikata mkono wake wakati akijaribu kuvunja kioo kwenye mlango ili atoroke kabla ya polisi kuwasili katika eneo hilo.Alitekwa siku ya jumamosi na watu waliokuwa wamefunika nyuso zao wakati akitokea kwenye sherehe moja karibu na mji wake anaoishi wa Ciudad Victoria katika jimbo la Tamaulipas.

No comments: