Tuesday 4 October 2016

mamilion ya pesa yakutwa yamechimbiwa chini Arusha



Image result for tanzanian shillingIlikuwa ni tafrani katika mtaa wa mianzini jijini hapa leo wakati mradi wa utanuzi wa barabara kutoka mianzini kwenye mataa hadi ilding’a ukiendelea, Tingatinga lililokuwa likifanya kazi ya kutanua barabara hiyo lilipochimbua mfuko wa plastiki uliokuwa umesheheni  minoti ya hela  uliokuwa umechimbiwa chini kwenye nyumba moja ya matope iliyokuwa imebomolewa kupisha utanuzi wa barabara hiyo.

Katika hali ya kushangaza jijini Arusha eneo la Mianzini yamepatikana mamilioni ya hela yakiwa yamefukiwa chini  ya Ardhini.
Katika eneo la tukio ilikuwa ni sherehe na vifijo kwa wapiti njia waliokuwa wakijitafutia riziki lakini ilikuwa kilio kwa familia ya mzee Christopher Akoonay alimaarufu kwa jina la “MBULU” ambaye inasemekana ni mmiliki wa nyumba iliyobomolewa kupisha utanuzi wa barabara hiyo .
Akoonay hujishughulisha na ufugaji wa ng’ombe wa maziwa na hufanya biashara ya kusambaza maziwa katika jiji la Arusha na viunga vyake, Alizungumza na Mwandishi wetu kwa njia ya simu mzee Akoonay alitueleza “ Nikweli hela ni zangu na nyumba iliyobomolewa ni yangu “ alisema Akooney , hakuishia hapo aliendelea kusema anashangaa wajenzi wa barabara hiyo kubomoa nyumba yake kwani yeye na baadhi ya wananchi walifungua shauri mahakamani kudai fidia endapo nyumba zao zitabomolewa kabla ya mradi wa barabara kupita hapa” lakini kesi ilitupiliwa mbali na mahakama , wajenzi hawakusubiri hata lisaa walianza moja kwa kubomoa nyumba zetu hata nikiwa sijatoa baadhi ya vitu vyangu ndani.
Christopher Akoonay alipoulizwa kwanini hakupenda kuweka hela zake benki alisema “ nilikosa imani na benki maana wakati nikifanya kazi kama mtumishi wa serikali miaka ya 1980 nilikuwa nina akaunti benki baada ya kustaafu mwaka 1994 nikaamua kujishughulisha na shughuli za ufugaji sikufuatilia akaunti yangu baada ya kustaafuhadi ilipofika mwaka 2000 nilikwenda kuangalia fedha zangu benki nikaambiwa kwasababu nimekaa zaidi ya miaka 10 napaswa kwenda benki kuu kujieleza kwa nini sikutumia akaunti hiyo kwa mda mrefu , nkaona huo ni usumbufu sikufuatilia na ndipo nilipopoteza imani na benk na kuamua kujihifanyia fedha zangu nyumbani
Baadhi ya wananchi wa eneo hilo walipo hojiwa na mwandishi wetu , wakizungumzia swala hilo kwa masharti ya kutotajwa majina yao wamesema wanashangazwa na Akoonay kuwa na kiasi kikubwa cha fedha kiasi kikubwa namna hiyo na kuzifukia chini ya aridhi wakati anaishi kwenye nyumba ya matope.

No comments: