Thursday 6 October 2016

Walimu waliokuwa mazoezini waliomchapa mwanafunzi watiwa mbaroni.



Waziri wa mambo ya ndani nchini Mh. Mwigulu Nchemba aliwaagiza maafisa kuwasaka waalimu watatu wa mafunzo ambao wanadaiwa kumpiga mwanafuzi mmoja aliyefahamika kwa jina la Sebastian Chinguku anayesoma kidato cha tatu katika shule ya sekondari Mbeya day iliyoko jijini Mbeya.

mwalim Frank
Walimu waliompiga mwanafunzi huyo walijulikana kwa majina Mwalimu  Sanke Gwanaka kutoka chuo kikuu cha mwalimu Nyerere Memorial kilichoko Dar Es Salaam na Frank Msigwa , na john Deogratius kutoka chuo Kikuu cha Dar es salaam ( UDSM). Inadaiwa waalimu hao wakiwa katika mafunzo yao ya vitendo , mwalim Frank alitoa zoezi la somo la kiingereza ambao baadhi ya wanafunzi walimgomea kufanya zoezi hilo akiwemo mwanafunzi Sebastian. mwalimu huyo alianza kuwashambulia wanafunzi kwa viboko ndipo Sebastian akahoji kwanini anapigwa , mwalimu alianza kumshambulia kwa kumpiga makofi baadae alimpelaka staff room ( ofisin ) ambako waalimu walianza kumshambulia kwa kumchapa na mwalimu Frank alianza kumpiga vibao na kumkaba koo .
Tangu hapo baada ya mwanafunzi kuachiliwa alipotea shuleni na kutokomea na waalimu hao walirudi vyuoni kwao.



 Angalia video ya waalimu hao wakimshambulia mwanafunzi huyo
Akizungumza na waandishi wa habari waziri wa mambo ya ndani Mh. Mwigulu Nchemba amedai uchunguzi wa awali unaonyesha tukio hilo lilitokea mnamo tarehe 28 september 2016. Pia walimu wote wanaodaiwa kuhusika na tukio hilo wanashikiliwa na jeshi la polisi , pia jeshi la polisi mkoani huko wanaendelea kufanya mahojiano na uongozi wa shule ya sekondari Mbeya Day 

 

No comments: