Tuesday 24 January 2017

Bombadier ya ATCL yatua Mwanza baada ya kupata dharura Mwanza

Ndege ya Bombardier Q400 ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) iliyokuwa ikitoka Mwanza kwenda Dar es salaam jana ililazimika kutua katika uwanja wa ndege wa Mwanza dakika ishirini baada ya kuanza safari yake. Ndege hiyo iliyoruka kutoka uwanja wa ndege wa Mwanza kwa safari ya kuelekea Dar es salaam saa mbili asubuhi, ililazimika kutua kwa dharura uwanjani hapo dakika 20 baadae kwa ajili ya kurekebisha dharura ambayo mpaka muda huo ilikuwa haijafahamika. Rubani aliwataarifu abiria kuwa wanalazimika kutua uwanjani hapo kwa sababu ya dharura iliyojitokeza. Baada ya wataalamu kuikagua ndege hiyo waligundua kuwa mlango wa sehemu ya kuwekea mizigo haikufungwa kitukilichopelekea taa ya kuashiria hatari kuwaka na kumlazimu rubani wa ndege hiyo kulazimika kutua kwa dharura.

No comments: