Tuesday 28 February 2017

Mbowe atinga mahakamani kusikiliza kesi ya Lema


Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Mhe. Freeman Mbowe akiwa ameongozana na Mbunge wa Kibamba wakiwasili katika Mahakama Kuu Mkoa wa Arusha Leo Jumatatu 27/02/2017 ikiwa leo linasikilizwa shauri la Mbunge wa Arusha mjini, Mhe. Godbless Lema.
Viongozi wengine waliofika mahakamani leo ni Katibu Mkuu wa CHADEMA Taifa, Dkt. Vincent Mashinji, Mjumbe wa Kamati Kuu,Prof. Mwesiga Baregu, Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Frederick Sumaye, Meya wa jiji la Arusha,Mhe. Calist Lazaro, Katibu wa CHADEMA Arusha, Mhe. Aman Golugwa na viongozi mbalimbali wa CHADEMA

No comments: