Friday 10 February 2017

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) jela miaka mitano kwa matumizi mabaya ya madaraka.

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuhukumu kifungo cha miaka mitatu jela au kulipa faini ya Sh milioni 5, aliyekuwa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Ephraim Mgawe kwa mashitaka ya matumizi mabaya ya madaraka.
Hata hivyo, Mgawe ameachiwa huru baada ya kulipa faini hiyo.
Mashitaka aliyokuwa anashitakiwa nayo ni ya upanuzi wa Bandari ya Dar es Salaam gati namba 13 na 14 kwa Sh trilioni moja mkataba walioingia na kampuni ya ujenzi ya China Communication Construction Company Limited (CCCCL).
Aidha, mahakama hiyo ilimwachia huru  aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi wa TPA, Hamadi Koshuma baada ya upande wa mashitaka kushindwa kuthibitisha mashitaka dhidi yake.

No comments: