Tuesday 4 April 2017

Mchekeshaji kutoka ufaransa aamua kuatamia mayai kwa siku 21

Msanii kutoka Ufaransa Abraham Poincheval anaendelea kuatamia mayai ya kuku akiwa na matumaini kwamba mwishowe yataangua vifaranga.
Msanii huyo anatumia joto kutoka kwa mwili wake kutamia mayao hayo 10.
Poincheval ambaye hufanya uigizaji wa kuigiza mambo ya ucheshi lakini ya hatari tayari ameishi wiki mbili ndani ya dubu, miongoni mwa mambo mengine ya kushangaza.
Atakuwa katika chumba maalum ambacho anatamia mayai, ambapo watalii wanaweza kumtazama katka makumbusho ya Palais de Tokyo mjini Paris.
Anatarajia kutamia mayai hayo kwa siku 21 hadi 26.

No comments: