Thursday 18 May 2017

Kikwete ateuliwa kuwa mwenyekiti mwenza wa baraza la wakimbizi duniani

Aliyekuwa rais wa Tanzania Mh. Dr. Jakaya Mrisho Kikwete ameteuliwa kuhudumu katika baraza kuu la wakimbizi duniani WRC, ambalo ni kundi huru la viongozi na wavumbuzi wanaolenga kubuni mbinu mpya za kutatua mizozo ya wakimbizi.
Kulingana na gazeti la The Citizen nchini Tanzania, taarifa kwa vyombo vya habari ilimtaja Bwana Kikwete kuwa mwenyekiti mwenza wa baraza hilo lililopo chini ya uenyekiti wa waziri wa maswala ya kigeni nchini Canada Lloyd Axworthy.
Gazeti hilo limesema kuwa Hina Jinali kutoka Pakistan na Rita Sussmith kutoka Ujerumani watafanya kazi pamoja na bwana Kikwete kama wenyekiti wenza huku Paul Heinbecker akichaguliwa kama naibu huku naye Fen Hamson akihudumu kama mkurugenzi.
Taarifa hiyo imesema kuwa miongoni mwa mengine, baraza hilo litatoa ushauri wa marekebisho na uvumbuzi ili kuimarisha mfumo wote wa wakimbizi duniani.
Baraza hilo litaleta mabadiliko ili kusaidia kuhakikisha kuwa ushirikiano wa kimataifa kwa wakimbizi unaeleweka, unafanyika kwa njia ya usawa na haki, ilisema taarifa hiyo.
Baraza hilo pia litashirikisha madiwani 17 wa mabaraza.

No comments: