Thursday 14 December 2017

ASKARI AMPIGA RISASI ASIKARI MWENZIE KWA WIVU WA MAPENZI

Akizungumza na waandishi wa habari mtu wa karibu na askari hao amesema kuwa chanzo cha ugomvi wa askari hao ni wivu wa mapenzi ambapo marehemu pamoja na mtuhumiwa ambaye ametambulika kwa jina la Faustine Masanja wameona nyumba moja.

Amedai marehemu alipofika asubuhi kazini ndipo mtuhumiwa Masanja alimpiga mwenzake risasi ya kichwa na alipokimbizwa katika hospitali ya Mkoa Mount Meru alifariki dunia.



ASKARI magereza Faustine Masanja amemuua askari mwenzake Ombeni Mwakiyani kwa kumpiga risasi kichwani.

Kamanda wa mkoani hapa, Charles Mkumbo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo lililotokea leo majira ya asubuhi wakati wakiwa kazini kwenye gereza la mkoa la Kisongo.
Mmoja wa mashuhuda tukio hilo ambaye hakuwa tayari jina lake kuandikwa alisema kuwa askari Masanja alimpiga risasi mwenzake wakiwa wanawapakia mahabusu kwenye gari kwa ajili ya kuwapeleka kwenye mahakama mbalimbali za mkoani hapa kwa ajili ya kusikiliza kesi zao.

"Masanja alikuja akampiga Ombeni risasi ya kichwa kwa nyuma ikatokea usoni alipomaliza akatupa silaha chini akasema sikimbii nikamateni kwa kuwa najua nimeua," alisema shuhuda huyo.

Hata hivyo baadhi ya askari magereza ambao hawakuwa tayari majina yao kuandikwa walidai kuwa Ombeni na Masanja wake zao ni ndugu hivyo kuna uwezekano kulikuwa na mgogoro wa kifamilia.

SOURCE: http://www.habaritanzaniagracemacha.com/

No comments: